Monday 27 June 2016

Unknown

NYLON GUITAR KWA MAMTAG AWARDS - TUMPIGIE KURA P DAY AKUJE NA TAJI NYUMBANI.


Kuwa msanii hapa mombasa huwa ni changamoto kubwa haswa ikija wakati wa kupata airplay na "support" kutoka kwa mafans. Naamini kitambo mashabiki wakukubali huwa umewagusa nyoyo zao kwa kupitia mziki unaofanya kama msanii.
Wengi hujitumbukiza kwa dimbwi la sanaa ambapo baada ya muda hivi wanajipata nje ya mduara wa wale wanaoendelea kisanaa. Hio inakuja pale mtu anafanya mziki bila malengo. Msanii kuwa na malengo yake kisha kufanya sanaa yake ndani ya malengo yake hapo ndo utapata manufaa ya sanaa yanajitokeza pole pole. Hakuna mtu alianza na kuwa nyota tayari hivyo basi changamoto ya ku "maintain strategies" zako kama msanii ndo hufanya wengine wanabuma.

Leo nimeamka na hii post ya huyu msanii, hebu angalia alichoandika;



"hi guys, my song "nylon guitar" iz nominated the best afro fusion song of year..."Mamtag awards".to vote for me ...dial,*868*2263# n follow the procedure.
Ur my famly ,my everything..
#‎surpotpday"


Nikikumbuka vizuri hii nyimbo NYLON GUITAR ilitoka 2015, airplay yake ilikua chini sana japo mashabiki walijitahidi sana. Nyimbo hio hio sasa imeekwa kwa MAMTAG AWARDS kama BEST AFRO FUSION SONG OF THE YEAR.

Hii ni dhalili ya kuwa nyimbo nzuri haipotei. Hivyo basi tujitahidi kumpa ndugu yetu support ili alete taji hilo nyumbani mombasa.
 Unaeza pata kuuskiza wimbo huo kwa mkito, waptrick na pia youtube.

KWA KUMPIGIA KURA  BONYEZA *868*2263# KISHA UFWATE MAELEZO.

#SUPPORTPDAY

Subscribe to get more videos :