Thursday 29 November 2018

Unknown

Mziki wangu UnaKIKI tosha. Situmii KIKi kuongelewa Mitandaoni na Magazetini. Sudi Boy Afunguka.


Msanii wa mziki wa kizazi kipya kanda ya pwani sudi boy amesema kutengeneza kiki ili kujipatia umaarufu sio mambo yake.

Akipiga gumzo na #KayaFlavaz, Sudi Boy amesema kuwa aina ya mziki anaofanya una kiki za kutosha kwa hiyo sio lazima kuzua au kutengeza matukio kama wasanii wengine wafanywavyo ili kuongelewa mitandaoni.

Sudi boy ambaye kwa sasa anatamba na kibao 'nalo' alichomshirikisha arrow boy, ametumia fursa hiyo kuchomoa wimbo mpya kwa jina Kamelodi kama kasi ya kumalizia mwaka.

Skiza Nyimbo Mpya Kamelod hapa
Kamelod MP3

Source: KayaFlavaz.

Tags: Dada Viva #LeoBurdani

Subscribe to get more videos :