Thursday 16 June 2016

Unknown

JE CHID BENZ HUENDA AKAACHILIA WIMBO WAKE STUDIO ZA WASAFI?


Miezi michache tu baada ya nyota wa bongo fleva CHID BENZ Kupatikana akiwa kwa hali mbaya ya kiafya baada ya kutumia dawa kupitiliza, na kupelekwa rehab na manager Babu Tale, kisha habari za yeye kutoroka rehab kuchipuka baada ya kuondoka na Babu Tale wakati amemtembelea habari ambazo yeye pamoja na Manager huyo walizipuuzia na kuzitupilia mbali kuwa za uongo na uzushi.
Hivi sasa Chid Benz mkali wa Ilala yuko imara na afya yake inazidi kuimarika kwa hali ya juu zaidi.
Kuonekana kwake kwa studio za wasafi kuimeibuka hadisi kibao kwani wengi wanajiuliza kwani vipi, Chid ndio "NEXT" baada ya Mavoko?
Picha ya hapo juu inaonesha akiwa na mmoja ya wale wakali wa studio hizo. Tazama picha zengine hapa; -

Chid Benz baada ya kutoka rehab.


Chid Benz kabla ya kupelekwa Rehab.

Chid Benz akiwa na Babu Tale.

Subscribe to get more videos :